Ufafanuzi zaidi Mabasi Kushusha Abiria Wagonjwa Hospitali ya Ikonda (Video)


 Siku chache kabla ya agizo la mabasi ya abiria kutakiwa kuanza kuitumia stendi ya mabasi Tandala wilayani Makete mkoani Njombe, ufafanuzi wa baadhi ya mambo ikiwemo kushusha na kupakia abiria umetolewa na Halmashauri hiyo

 

Katika mahojiano maalum na mtandao huu ofisini kwake, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo William Makufwe amesema pamoja na kwamba mabasi yanatakiwa kushusha na kupakia abiria katika stendi ya Tandala, lakini endapo kuna abiria wagonjwa waliopo kwenye basi husika watawaruhusu kwenda kuwashusha hospitali ya Ikonda na basi hilo kurudi stendi ya Tandala


Hiyo ni kutokana na sintofahamu iliyojitokeza kwa baadhi ya watu baada ya tangazo la kuanza kutumika kwa stendi hiyo ya Tandala kuanzia Oktoba 1, 2022, hivyo kituo hiki kikataka kufahamu kuhusu baadhi ya abiria wagonjwa kushushiwa stendi ya Tandala badala ya Ikonda hospitali, ambapo amesema hilo litaruhusiwa huku akitoa onyo kwa wanaopotosha taarifa za matumizi ya stendi hiyo Kwa kuwa upo uwekezaji uliofanyika katika eneo hilo hivyo inatakiwa kuanza kutumika


Amesema kuanza kutumika kwa stendi ya mabasi Tandala ni utekelezaji wa agizo la muda mrefu wa vikao vya madiwani wa Halmashauri hiyo ikiwemo Kamati ya Fedha ambapo walikubaliana kuifufua stendi hiyo ili ianze kutumika.


Bofya hapo chini kuona video hiyo   


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo