Akizungumza Mahakamani hapo, leo Mei 10, Hakimu Mkazi, wa
mahakama hiyo, John Mpitanjia amesema amepokea vielelezo hivyo
baada ya kupitia sheria mbalimbali za mitandao ya kijamii.
Mpitanjia amesema, mahakama inawajibu wa kupokea kila kielelezo
kinachokuja mbele yake.
Baada ya uamuzi huo upande wa utetezi chini Wakili Chance Luoga
uliridhia maamuzi hayo na kuomba kesi hiyo iendelee tena Mei 14
Nondo ambaye pia ni Mwenyekiti wa Mtandao wa Wanafunzi wa Vyuo
Vikuu,(TSN) anakabiliwa anakabiliwa na mashtaka mawili shtaka la
kwanza ni kusambaza taarifa za uongo akiwa jijini Dar es Salaam kuwa
ametekwa na kosa la pili ni kutoa taarifa za uongo akiwa mjini Mafinga
kwa askari Polisi kituo cha Mafinga Wilayani Mufindi.
