Mkuu wa Mkoa wa Singida, Rehema Nchimbi amegoma kukaa
eneo alilotengewa mgeni rasmi kwa kile alichodai hawezi kukaa kivulini wakati watoto wanakaa juani.
Tukio hilo limetokea leo, Mei 14, wakati Nchimbi akizindua wiki ya elimu inayofanyika kitaifa wilayani Mkalama mkoani Singida.
Nchimbi amechukua hatua hiyo baada ya kupokea maandamano ya shule mbalimbali wilayani humo na kuona watoto wote wamesimama juani.