Mwenyekiti UVCCM: Simfahamu Mtu Anayejiita Mange Kimambi

Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), (UVCCM), Kheri James amefunguka na kusema yeye hamtambui wala kumjua mwanaharakati wa mitandaoni Mange Kimambi na kusema angekuwa anamtambua angeweza kumzungumzia.

Kheri James amesema hayo alipokuwa kwenye kipindi cha Kikaangoni kinachorushwa na kituo cha  EATV.

Mbali na hilo Kheri James alidai kuwa yeye hatambui wala kufahamu juu ya maandamano ya nchi nzima ambayo yanahamasishwa kupitia mitandao ya kijamii ambayo yanadaiwa kufanyika April 26 mwaka huu.

Hata hivyo Mwenyekiti huyo wa wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi, Kheri James amewalalamikia baadhi ya watanzania na wapinzani ambao wamekuwa wakiisema na kuitangaza nchi kwa mambo mabaya yaliyopo ndani

Amesema  jambo hilo ni baya sana kwani litaleta athari kubwa kwani wawekezaji, watalii watahofia kufika nchini  kwetu jambo ambalo litafunga milango ya maendeleo ya nchi.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo