Walimu wapigwa marufuku kujihusisha na siasa mashuleni

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Siha, Valerian Juwal amewaonya walimu wa shule za msingi na sekondari kutojihusisha na masuala ya vyama vya kisiasa mashuleni.
Tokeo la picha la Valerian Juwal siha
Valerian Juwal
Valerian amesema kuwa walimu kujihusisha na masuala ya kisiasa wakiwa mashuleni kunapelekea walimu kushindwa kufikia malengo yao.
Walimu acheni tabia ya kujiingiza kwenye vyama vya kisiasa na kuacha majukumu yenu ambayo yapo kwa mujibu wa sheria na taratibu za ajira kwa kuwa mnapopatwa na matatizo hakuna wa kuwatetea zaidi ya mwajiri,“amesema Juwal kwenye mkutano mkuu wa Chama cha Walimu wilayani Siha uliofanyika Jumanne ya wiki hii.
Kwa upande mwingine, Afisa Elimu Msingi wa Wilaya ya Siha, Rose Sandi amesema kwa walimu kujiingiza kwenye masuala ya kisiasa kunaweza kupelekea kuporomoka kwa kiwango cha ufaulu kwa wanafunzi.
Kwa mujibu wa sheria ya utumishi wa umma ya mwaka 2009, inamtaka mtumishi yeyote wa umma kuwa na nidhamu na kutojihusisha na masuala ya siasa, hivyo kwa kufanya hivyo ni kuvunja sheria.
Chanzo:Nipashe


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo