Ole Sosopi: "Nitaongoza msafara kesho'

Mwenyekiti wa Baraza la Vijana CHADEMA, BAVICHA, Patrick Ole Sosopi amefunguka na kusema kesho Jumapili April 1, 2018 ataongoza msafara wa viongozi wa BAVICHA kwenda kuwaona viongozi wao sita ambao wapo mahabusu Segerea

Ole Sosopi amesema hayo leo alipokuwa akiongea na waandishi wa habari na kusema kuwa Katibu Mkuu wa BAVICHA yeye ataongoza viongozi wa Baraza hilo la vijana Mbeya kwenda kuwaona Mbunge wa Mbeya Mjini Joseph Mbilinyi na mwenzake Katibu wa CHADEMA Kanda ya nyanda za juu kusini, Emmanuel Masonga ambao wamefungwa katika gereza la Rwanda Mbeya. 
"Mimi kama Mwenyekiti nitaongoza msafara wa viongozi wa BAVICHA katika level zote kwa mkoa wa Dar es Salaam kuelekea gereza la Segerea kesho kuwatembelea viongozi wetu lakini pia Katibu Mkuu na Muhamasishaji Vijana Taifa wao wataelekea Mbeya kwa ajili ya kumtembelea kamanda Sugu na Masonga katika kipindi hiki cha mapumziko tutafanya shughuli zetu kwa kuwatembelea makamanda wetu na kuwatia moyo na kuwaeleza kwamba mapambano huku nje yanaendelea japo wao wapo magerezani" alisema Sosopi 
Viongozi sita wa CHADEMA akiwepo Mwenyekiti wa chama hicho, Katibu Mkuu Dkt. Mashinji, Mbunge Msigwa, Mbunge John Mnyika, Mbunge Ester Matiko na Salum Mwalimu wapo mahabusu licha ya Mahakama kuwapatia dhamana toka Alhamisi  hata hivyo watasalia rumande hadi kesi yao itakapotajwa tena wiki ijayo tarehe 3 Aprili ambapo wataletwa mahakamani kukamilisha masharti ya dhamana.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo