Diwani akamatwa kwa kutapeli watu kwa kuwauzia ardhi ya Serikali

Mwanamke mmoja anayejulikana kwa jina la Halima Salum (51) ambaye pia ni diwani wa Fuoni Unguja, amekamatwa na polisi kwa tuhuma za kuwauzia watu ardhi ya serikali na kuwatapeli fedha zao kutokana na watu hao kushindwa kuitumia ardhi hiyo kwani ni mali ya Serikali.
Akithibitisha kukamatwa kwa mwanamke huyo Kamanda wa polisi mkoa wa mjini magharibi Unguja Hassan Nassir amesema walimkamata akiwa na mwenzake aliyejulikana kwa jina la Idrisa Mwinyi Khamiss ambao kwa pamoja waliuza kipande cha ardhi huko Fuoni Kibondeni kwa Tsh. 6,000,000 ambapo mnunuzi alishindwa kufanya shughuli yeyote katika eneo hilo baada ya kubaini kuwa ni eneo la Serikali.
Wakati mwanamke huyo akiwa mikononi mwa polisi kwa upelelezi alitokea kijana Salum Saleh (28) naye pia alitoa malalamiko kwa polisi kuwa mwanamke huyo alimuuzia  kipande cha ardhi ambacho si mali yake wala ya Serikali kwa zaidi ya Tsh. 2,000,000.
Katika kuitikia wito wa Serikali kutaka kuondoa migogoro ya ardhi nchini Kamanda Nassir amesema hawatosita kumchukulia hatua mwanamke huyo bila kujali cheo chake ili kutokomeza migogoro ya ardhi nchini.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo