CHADEMA Wafunguka Diwani wao Kukimbilia CCM

Image result for mwenyekiti wa chadema makete

Siku moja baada ya kujiuzulu diwani wa Isapulano kupitia CHADEMA NA kisha akajiunga na CCM Mh Alphonce Mbilinyi, mwenyekiti wa Chama cha demokrasia na maendeleo CHADEMA Wilaya ya Makete Ibrahim Ngogo amezungumzia uamuzi wa kiongozi huyo kuhamia CCM na kusema walikuwa mbioni kumtimua

Mwenyekiti huyo amesema walimuita marakadhaa katika chama chao na kumuonya kutokana na mwenendo wake usioridhisha na akaahidi kuyatendea kazi maagizo hayo, lakini amejiuzulu kabla ya kikao kingine kilichopangwa kufanyika Aprili mwaka huu ambacho kilikuwa kimtimue kwenye chama hicho endapo kusingekuwa na mabadiliko yeyote

Ngogo amesema huwenda diwani huyo amekimbilia CCM kwasababu aliogopa kutimuliwa kwenye chama chao, na kusema pamoja na yote aliyoyafanya, uchaguzi mdogo wanaimani CHADEMA itashinda kama uchaguzi utakuwa huru na wa haki


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo