Ajali ya basi La New Force yaua watano na kujeruhi

Basi la abiria kampuni ya New Force limegongana na basi dogo la abiria aina ya hiace na kupelekea vifo vya watu watano na kujeruhi watu wengine tisa, ajali hiyo imetokea leo Machi 4, 2018 majira ya saa nne asubuhi

Basi la New Force lilikuwa linatokea Msamvu kwenda Mikese liligongana na gari dogo la abiria (Hiace) lililokuwa linatokea Msamvu, mkoani Mogororo.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Morogoro, Urich Matei amethibitisha kutokea kwa ajali hiyo na kusema kuwa watu watano wamefariki dunia huku wengine 9 wakiwa wamejuruhiwa na wanaendelea kupatiwa matibabu katika hospitali ya Morogoro. 
Kwa mujibu wa mashahuda wa tukio hilo wamedai kuwa chanzo cha ajali hiyo ni dereva wa hiace ambaye alikuwa akitaka kulipita gari la mchanga lililokuwa mbele yake hivyo akajikuta amegongana uso kwa uso na basi hilo.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo