TANESCO Makete Yatoa Onyo Kali Kwa wafugaji wa aina Hii

 Ng'ombe akiwa amefungwa kwenye nguzo ya Umeme Makete mjini kama ilivyokutwa na Mwandishi wetu
Shirika la umeme TANESCO wilaya ya Makete limetoa onyo kali kwa wananchi hasa wafugaji ambao wamekuwa wakifunga mifugo yao kwenye nguzo za umeme ama kwenye nyaya zinazoshikilia nguzo hizo
Onyo hilo limetolewa na Meneja wa TANESCO wilaya ya Makete Bw. Henrico Renatus baada ya mwandishi wetu kukuta mwananchi mmoja mkazi wa Makete mjini katika Mji Mdogo wa Iwawa kufunga ng'ombe kwenye waya unaoshikilia nguzo ya umeme
Meneja huyo amelielezea tukio hilo ambalo lililalamikiwa na baadhi ya wananchi waliolishuhudia na kukiri kupokea malalamiko hayo lakini hakuwa tayari kumtaja mwananchi huyo aliyefanya hivyo
Ameelezea hatari inayoweza kutokea kwa wananchi kufanya vitendo hivyo ikiwemo nguzo hizo kukosa uimara wake, pamoja na vikombe vinavyobeba nyaya kupasuka na kusababisha waya unaoshikilia nguzo kusafirisha umeme ardhini na kusababisha madhara makubwa kwa wananchi
Ikumbukwe kuwa vitendo vya kuchunga mifugo ovyo katika eneo la miji ni marufuku kwa mujibu wa sheria licha ya baadhi ya wananchi kuamua kukiuka sheria hiyo na kufunga mifugo kwenye nguzo za umeme licha ya kuwepo mabango yaliyoandikwa hatari kwa kumaanisha kukataza mwananchi kufanya chochote kwenye nguzo hiyo 


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo