Shekhe Kundecha afunguka wapinzani kukimbilia CCM

Mwenyekiti Jumuiya na Taasisi za Kiislaam nchini Tanzania, Shekhe Mussa Kundecha amefunguka na kuweka wazi kuwa kitendo cha baadhi ya viongozi upinzani kukimbilia Chama Cha Mapinduzi si kwamba wote wanakubali utendaji wa serikali ila hawana namna tu

Shekhe Kundecha amesema hayo wakati akiongea na mwandishi wa habari na kusema kuwa si kila mtu ambaye anakwenda CCM ameridhika na hali hiyo na kudai wapo watu wamekubali kwenda kwa kulazimika kufanya hivyo.
"Siyo kila kukubali ni kuridhika na hilo jambo kuna kukubali jambo kwa kulazimika kufanya hivyo, waswahili wanasema hivi mkono usioweza kuuvunja basi ubusu kwa hiyo akikikuta mtu unaubusu anaweza kusema umeridhika kwamba eti umeshindwa hatua ya kuufanya kwa hivyo kujisalimisha nao una busu tu, sasa si kila kubusu ni kuridhika na hilo jambo kwa hiyo watu wanaweza kuwa wanakwenda kule kwa sababu ya kulazimika hawana hawana njia ya kufanya lakini si ishara ya kuwa watu wanakubali kama unatafakari kwa umakini" alisema Kundecha 
Shekhe Kundecha ametoa kauli hiyo wakati ambao viongozi mbalimbali wa CHADEMA na vyama vingine vya siasa nchini wakiwa wamejizulu nafasi zao katika vyama vyao na kujivua uanachama wa vyama hivyo na kwenda Chama Cha Mapinduzi (CCM) kwa kauli ya kuunga mkono jitihada za serikali ya awamu ya tano na Rais John Pombe Magufuli.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo