"Polisi wamevamia Makao Makuu CUF" - Mtatiro

Mwenyekiti wa kamati ya muda ya uongozi CUF, Julius Mtatiro amefunguka na kusema kuwa jeshi la polisi likiwa na magari kadhaa limevamia na kuzingira Makao Makuu ya (CUF) Zanzibar na kudai mpaka sasa haijafahamika sababu ya polisi kuzingira ofisi hiyo


Mtatiro amesema hayo na kudai kuwa huenda kuna mpango wa kutaka kumkabidhi ofisi hiyo Mwenyekiti wa CUF ambaye anatambulika na Msajili wa vyama vya siasa nchini Profesa Lipumba na kudai wao wanaendelea kufuatilia kujua nini kimewapeleka pale polisi. 
"Polisi wakiwa na magari kadhaa, wameivamia Makao Makuu ya Chama cha Wananchi CUF Mtendeni, Zanzibar saa 12.10 jioni hii. Inaonekana/inahisiwa wana ajenda mbili; moja ni kuikalia makao makuu hiyo kimabavu ili kesho Jumatatu waikabidhi kwa Bwana yule ili kutekeleza mkakati maalum, au wana lengo la kuingia kimabavu na kuweka vitu hatari na kisha kuwakamata viongozi wa CUF na kudai walitunza vitu hatari ofisini hapo. Tunafuatilia jambo hili kwa ukaribu " Julius Mtatiro


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo