Ngedere wasababisha Madhara Kwa wakulima Ilevelo Makete




Kijiji cha Ilevelo wilayani Makete Mkoani Njombe huwenda kikakumbwa na upungufu wa chakula msimu huu, kutokana na ongezeko la Ngedere wanaoharibu mazao katika mashamba ya chakula yaliyolimwa na wananchi hao katika kijiji hicho
Wakizungumza na mwandishi wa Green Fm wananchi hao wamesema wanyama hao waharibifu wanazidi kuongezeka katika kijiji chao kila kukicha ambapo kwa sasa wanaharibu mahindi na Njegere mashambani
Edson Sanga mkazi wa kijiji hicho amesema tatizo hilo ni kubwa lakini kwa kiasi kikubwa limechangiwa na upandwaji miti hadi kwenye mashamba yaliyotengwa kwa ajili ya kilimo hivyo hata ufukuzaji wa wanyama hao umekuwa mgumu
Naye Bibi Sikujua Sanga amesema anaziona dalili za njaa katika kijiji chao huku akiiomba serikali kuchukua hatua zaidi katika utekelezaji wa agizo la kuondolewa miti ya mbao kwenye mashamba ya kilimo
Mwenyekiti wa kijiji cha Ilevelo Bw. Seso Mahenge amezungumzia suala hilo na kusema Wao kama Kijiji hawajakaa kimya kukabiliana na tatizo hilo
Pia amesema wanapeleka ombi lao katika idara husika iliyopo halmashauri ya wilaya ya Makete kuomba msaada zaidi wa kuwafukuza wanyama hao ili kuepuka madhara yatakayowapata wananchi wake ambao wengi wao wanategemea mazao waliyoyalima shambani kujikimu kimaisha


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo