Wahalifu 6 Wakamatwa pamoja na Mbwa wao 14

Katika kupambana na watumiaji na wasambazaji wa dawa za kulevya pamoja na pombe za kienyeji Kituo cha polisi Mwera kimefanikiwa kuwakamata watu 6 wakiwa na lita 720 za maroweko ya pombe za kienyeji.
Akitoa taarifa hiyo kwa waandishi wa habari Kamanda wa polisi mkoa wa mjini magharib Unguja Hassan Nassir ali amesema vijana hao wanajiita mbwa mwitu walikamatwa huko Ndunduke wakiwa na lita 720 za maroweko ya pombe za kienyeji, Matangi 7 pamoja na Mbwa wao 14.
Vijana hao ni Omar Haji Makame (20) na Rashid Kheir Haji (19) wa Mtoni Kidatu , Hassan Haji Moh’d (18) na Ali Mzee Othman (20) wa Kwamtipura, Silima Bakari Silima (18), na Sleimani Juma Ali(29) wa Shaurimoyo.
Kamanda Nassir amesema wamegundua kuwa Ndunduke ndani ya eneo la msitu wa Masingini kumegeuzwa maficho ya wahalifu hivyo  watahakikisha vijana hao wanaeleza matukio yote ya kiuhalifu yanayofanyika na kusema watawapiga risasi Mbwa waliowakutanao kutokana na ushahidi kuonesha kuwa Mbwa hao walikuwa wakitumika kihalifu kwa kuwakamata raia wema na kuwapora mali zao.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo