Mambosasa aweka wazi mauaji kiongozi CHADEMA

Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Lazaro Mambosasa amefunguka na kusema kuwa jeshi la polisi linazo taarifa za watu walioshiriki mauaji ya kiongozi wa (CHADEMA) katika Kata ya Hananasif, Daniel John ambaye aliuawa na watu wasiojulikana

Kamanda Mambosasa akiongea na waandisha wa habari leo kutoa tathamini ya ulinzi na usalama katika kipindi cha uchaguzi wa marudio katika jimbo la Kinondoni amesema kuwa mpaka sasa wanazo taarifa za watu ambao wameshiriki kufanya mauaji hayo. 
"Jeshi la polisi kanda maalum linazo taarifa za watu walioshiriki katika mauaji ya mtu mmoja ambaye mwili wake uliokotwa na baadaye kujulikana kwamba ni ndugu Daniel John Mwenyekiti wa Kata ya Hananasifu ambaye mwili wake uliokotwa ukiwa umetupwa maeno ya fukwe za Coco beach, taarifa bahati nzuri tumeletewa na watoa taarifa wakielezea sakata zima la mauaji haya yalivyofanyika na kwa sababu tayari tunazo taarifa tunaendelea kufuatilia ili kuhakikisha wahusika wanakamatwa ili waweze kuhojiwa na kufikishwa kwenye vyombo vya mahakama kujibu tuhuma ambazo zinaendelea" alisema Mambosasa 
Aidha Mambosasa amewaomba Watanzania wawe wavumilivu na kusema kuwa tukio hilo ni tukio la mauaji kama yalivyo mengine hivyo haki itatendeka kwani kwenye taratibu za upelelezi hakuna 'double standard' bali zinafuatwa taratibu na miongozo iliyopo kwenye masuala ya upelelezi. 
Februari 14, 2018 Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe alitoa taarifa juu ya kuuawa kwa kiongozi huyo wa CHADEMA ambaye mwili wake ulikutwa ukiwa na majeraha mbalimbali mwilini.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo