Jeshi la Polisi Kanda Maalumu ya Dar es salaam limewaonya wananchi ambao wanaojiandaa na maandamano yanayoratibiwa kupitia mitandao ya kijamii na kusema kwamba wasijaribu kufanya hivyo kwani wataingia kwenye matatizo makubwa
Akizungumza na leo na waandishi wa habari Kamanda Mambosasa amesema kwamba Watanzania wajiepushe na uchochezi huo wa watu wachache wa kutaka kuiingza nchi kwenye vurugu.
Aidha Mambosasa amesema kwa yeyote ambaye hatasikia onyo hilo kwa mkoa wa Dar es salaam asije kujutia kwa yatakayotokea kwani jeshi limejipanga vilivyo na kwamba kwa sasa liipo kwa ajiili ya kutengeneza mazingira rafiki kwa wawekezaji.
"Kuna watu ambao wanaendelea kuhamasisha wananchi kuvunja sheria. Wanataka wajiandae kwa maandamano, tarehe wanazoendelea kutaja. lakini wanafanya hivyo wao wakiwa wamekaa sehemu salama. Wanataka kuwaingiza watanzania wengine kwenye shida,". Mambosasa.
Kumekuwa na vuguvugu la kufanyika maandamano Aprili 26 huku Mwanaharakati wa mitandaoni Mange Kimambi akionekana kuwa mstari wa mbele katika uhamasishaji.
