Mapato ya Halmashauri ya wilaya ya Makete kuundiwa Tume

Baraza la madiwani wa halmashauri ya wilaya ya Makete mkoani Njombe linatarajia kuunda tume ya kuchuguza suala zima la Mapato ya halmashauri hiyo

Hatua hiyo inatokana na sababu mbalimbali ikiwemo kutopelekwa kwa wakati asilimia 10 za fedha za vijiji, pamoja na kupungua kwa mapato ya halmashauri kutokana na sababu mbalimbali zinazoelezwa na wataalamu pamoja na waheshimiwa madiwani

Baadhi ya madiwani wakizungumzia hoja ya makusanyo ya halmashauri katika baraza la madiwani hii leo, wametoa maoni yao ikiwemo kupendekeza utaratibu uliokuwa ukitumika mwanzoni wa watendaji kupeleka mapato urudishwe ili iwe rahisi kupatiwa asilimia za vijiji


Mweka hazina halmashauri ya wilaya ya Makete Edward Mdagachule amelazimika kutolea ufafanuzi hoja hizo ikiwemo kutopelekwa asilimia 10 za vijiji ambapo amesema mpaka sasa deni wanalodaiwa na vijiji ni Zaidi ya shilingi milioni 92 huku akitaja sababu za kutokulipa kuwa ni kutokana na mapato kuwa madogo kuliko matumizi

Amesema fedha zinazopatikana zimetumika kulipia posho za madiwani, mishahara ya watumishi wanaolipwa kutoka vyanzo vya mapato ya halmashauri, kununua mashine za makusanyo ya mapato (POS) 37, kulipia timu mbalimbali za uchunguzi, kulipia shughuli mbalimbali za utawala, pamoja safari za watendaji wa halmashauri

Hali hiyo ikamfanya mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya Makete Mh Egnatio Mtawa kudhamiria kuunda tume ya uchunguzi itakayofanya kazi kikamilifu kuhakikisha suala la mapato ya halmashauri linarejea katika mstari wake

sikiliza sauti hii


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo