Makete yatoa kauli hii kuhusu Agizo la Rais Magufuli

Halmashauri ya wilaya ya Makete imesema haiwezi kuwa tofauti na agizo la Rais Dkt John Magufuli la kukataza michango ilihali serikali inatekeleza elimu bure

Hayo yamesemwa na Afisa elimu msingi wilaya ya Makete Mwl Anthony Mpiluka wakati akitola ufafanuzi hoja ya michango katika baraza la madiwani wa halmashauri ya wilaya ya Makete

Amesema katika suala la michango wananchi wenyewe ndio watumie busara kukubali kuchanga kwa hiari yao au wakatae kwa sababu hakuna mtu wa kuwalazimisha

Pia amtumia nafasi hiyo kuwashauri wananchi wa kata ya Lupalilo wilayani hapa kufikiria namna ya kujenga shule nyingine ya msingi baada ya shule ya sasa kuwepo katika hifadhi ya barabara hivyo itabomolewa kupisha ujenzi wa barabara ya lami kutoka Makete hadi Njombe

Mwenyekiti wa halmashauri hiyo Mh Egnatio Mtawa ametaka tafsiri Zaidi itolewe kwa wananchi kuhusu tamko la Rais Magufuli ili lieleweke kwa lengo la kuboresha kiwango cha elimu kwa wilaya ya Makete

Msikilize akifafanua


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo