AUDIO: Kesi ya Mauaji Utweve Yamchefua RC Njombe, Atoa Maagizo

Mkuu wa mkoa wa Njombe Christopher Ole Sendeka akizungumza na wananchi wa Utweve Makete

Mkuu wa wilaya ya Makete Mh Veronica Kessy akizungumza kwenye Mkutano huo
Mwananchi akitoa kero yake kwa Mkuu wa Mkoa wa Njombe
Wananchi wakimsikiliza mkuu wa mkoa
Mkuu wa mkoa wa Njombe Christopher Olesendeka amesema atafuatilia hatma ya mauaji ya mtoto Fedi Atu Sanga (17) anayedaiwa kuuawa kwa kipigo mwaka 2016 katika kijiji cha Utweve kata ya Ukwama wilayani Makete

Ameyasema hayo baada ya kusikiliza kero za wananchi wa kijiji hicho hii leo, ambapo pamoja na mambo mengine wananchi hao wamesema hawaelewi namna kesi hiyo ilivyoendeshwa mpaka watuhumiwa hao wakaachiwa huru
Hali hiyo ikamfanya mkuu wa mkoa kuchukua maamuzi ambayo yameonesha kuwaridhisha wananchi wa kijiji hicho Kwa kumuagiza mwakilishi wa mkuu wa polisi katika ziara hiyo kuwasiliana na viongozi wake wampelekee nyaraka za kesi hiyo Ikonda
Akizungumza na wananchi, Mkuu wa mkoa amewahakikishia kuwa hatma ya kesi hiyo itajulikana kwa kuwa wao kama serikali watahakikisha sheria inafuatwa
Katika hatua nyingine mkuu huyo wa mkoa amewataka wananchi wa wilaya ya Makete kuanza kujenga utaratibu wa kuwafanyia tohara watoto wao wa kiume wakiwa wadogo kama njia mojawapo ya kupunguza kiwango cha maambukizi mapya ya virusi vya ukimwi
Sikiliza sauti hizo hapo chini:-


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo