Upigaji chapa Mifugo Makete, Mvua yatajwa kuuweka Usiku

Zoezi la kupiga chapa mifugo wilayani Makete mkoani Njombe linaendelea huku likionesha kufanikiwa kwa kiasi kikubwa

Akizungumza na blog hii Afisa Mifugo na Uvuvi wilaya ya Makete Bw. Aldo Mwapinga amesema tangu kuanza kwa zoezi hilo hivi karibuni, bado linaendelea kwenye kata mbalimbali za wilaya ya Makete

Amesema katika kata ambazo bado zoezi hilo kufanyika, hamasa inaendelea kutolewa kwa wafugaji na wananchi kuandaa vibanio kwa ajili ya kazi hiyo

Amesema pamoja na mafanikio ya zoezi hilo kasi yake inapungua kutokana na hali ya hewa ya wilaya ya Makete kwa sasa ambapo mvua zinaendelea kunyesha na zoezi hilo hutegemea zaidi jua hivyo wakati mwingine linaathiriwa na hali ya hewa ya mvua
Msikilize zaidi kwenye sauti hapo chini akielezea kwa kirefu


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo