Ufafanuzi Mwanasheria Kuhusu Makosa ya Mahakama Kuu kusikilizwa kwenye mahakama ndogo

Imeelezwa kuwa suala la mtuhumiwa kushikiliwa na jeshi la polisi na kufikishwa mahakamani kujibu shitaka au mashitaka yanayomkabili na kuelezwa kuwa upelelezi bado haujakamilika, ni suala la kisheria

Katika mahojiano maalum na eddy blog mwanasheria wa halmashauri ya wilaya ya Makete Godfrey Gogadi amesema kwa mujibu wa sheria ya mwenendo wa makosa ya jinai, mtu anapotenda kosa anatakiwa kukamatwa na kupelekwa polisi ambapo atahojiwa na polisi watakapojiridhisha na kosa hilo baada ya uchunguzi wa awali watamfikisha mtuhumiwa mahakamani huku upelelezi zaidi ukiendelea baada ya shauri lake kufikishwa mahakamani

Katika hatua nyingine mwanasheria huyo ametolea ufafanuzi suala la mshtakiwa aliyetenda kosa na kupelekwa katika mahakama ambayo haina uwezo wa kisheria wa kusikiliza shauri hilo ambapo kwa mujibu wa sheria ya mwenendo wa makosa ya jinai kifungu cha 20 kinaeleza wazi kuwa makosa yote ya kijinai ambayo yanatakiwa yasikilizwe na mahakama kuu yahatapelekwa moja kwa moja mahakama kuu na badala yake yataanza na usikilizwaji wa awali kwenye mahakama za kwanza

Sikiliza sauti hapo chini kwa kubofya play:-


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo