Idadi ya watoto wasiojua KKK imepungua katika Halmashauri ya Tarime Mjini

Na Asha Shaban,Tarime.

Idadi ya watoto wasio jua kusoma na kuandika wa darasa la kwanza mpaka la tatu katika Halmashauri ya Tarime mjini mkoani mara imepungua   kutoka watoto 3268 mwaka 2015 hadi watoto 2628 mwaka 2017   kutokana  na kuwepo na vituo vya utayari  vilivyopo chini ya  mpango wakuboresha elimu Nchini Tanzania(EQUIP).

Akizungumza na wandishi wa habari walio tembelea Mradi huo hivi karibuni Afisa Elimu Msingi Daniel Makorere alisema kuwa idadi ya watoto  imeongezeka katika uandikishwaji kutoka watoto 9809mwaka 2015 hadi watoto 14,104 mwaka huu.

Aliongeza  kuwa vituo hivyo vya utayari vilianzishwa mahususi kutokana na watoto wengi kuanza darasa la kwanza kwa kutokuwa na msingi mzuri wa elimu ya awali kutokana na shule nyingi kuwepo mbali na makazi   hivyo kupelekea  wazazi wengi kushindwa kuwapeleka watoto wao katika shule za awali.

“ zipo sababu nyingi zilizo pelekea kuanzishwa kwa vituo hivyo kama  vile umabali wa kutoka  makazi ya watu mpaka zilipo shule na kuwepo kwa vijito vingi na milima ambayo kwa watoto wadogo hawawezi kwenda  shule hizo”Alisema

Kwa upande wake mratibu wa mafunzo EQUIP-TANZANIA mkoa wa mara Kiangi Elifadhi alisema mradi huu umedhaminiwa na DFID-UKAID  toka Uingereza na kuwa mradi huu upo katika shule zote za msingi  katika mikoa tisa ambayo ilikuwa chini kiufaulu.

Alisema mradi huu ni wa miaka sita ambapo kwa awamu ya kwanza walianza na mikoa ya Mara,Simiyu,Shinyanga,Tabora,Kigoma,Lindi na domama na kwa awamu ya pili mradi huu utafanya kazi na mikoa ya Singida na Katavi.

Aliongeza kuwa miradi hii yote inagarimu kiasi cha shilingi billion 184 ambapo kwa awamu ya kwanza uligarifu kiasi cha shilingi billion 136 na kwa mikoa milili iliyo ongezeka  itagarimu kiasi cha silingi billion 48 kwa mradi wa miaka miwili.

Elifadhi alisema kuwa wananchi wanajukumu la kuchangia katika ujenzi wa madarasa katika vituo hivyo vya utayari na inapokuwa shule shikizi basi mradi unaongezea nguvu kwa kutoa kiasi cha million 60 kwa kuongezea nguvu za ujenzi kwa kila kituo.

Kwa upande wake mratibu wa mpango wa utayari kuanza shule(SRP)Tabu Lazaro alisema kuwepo kwa vituo hivi 3 katika kijiji cha mogabiri kata ya kitare kumewezesha kwa kiasi kikubwa kwa watoto wengi kuweza kufika shule kwani vizuizi vilivyokuwepo awali vimepata ufumbuzi kwa watoto hao.


Aliongeza kuwa wazazi wamekuwa na mwamko wa kuwapeleka watoto wao katika vituo hivyo vya utayari na kuhamasika pia katika ujenzi wa vituo hivyo kwa kushindana katika mitaa yao kwani waliweza kugawana madarasa ya kujenga kwa mitaa hivyo kuweza kuhamasishana wao wenyewe.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo