Ndege yatua kwa dharura baada ya mke kumfumania mumewe

Ndege ya Qatar Airways ambayo ilikuwa ikitokea Doha kuelekea Indonesia ililazimika kutua kwa dharura India usiku wa manane kufuatia abiria mmoja mwanamke kuanza kumpiga mumewe akimtuhumu kumsaliti baada ya kufungua simu ya mumewe huyo wakati amelala.

Unaambiwa simu ya mume huyo ilikuwa na password ya fingerprints ambapo mwanamke huyo alitumia kidole cha mumewe akiwa amelala na kuifungua simu na kugundua mumewe huwa anamsaliti.

Baada ya vurugu hizo kuendelea Ndege ilitua Chennai, India kwa dharura kisha wakaamriwa kuteremka na kuwekwa kizuizini katika Airport kabla ya kusafirishwa kuelekea Kuala Lumpur.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo