Mtoto Humphrey Makundi aliyepotea akutwa amezikwa, Polisi wamfukua

Jeshi polisi mkoani Kilimanjaro linawashikilia watu kumi na moja akiwemo mmiliki wa taasisi ya elimu ya Scolastika kwa tuhuma za kuhusika na mauaji ya mwanafunzi wa kidato cha pili Humprey Makundi ambaye amebainika kufariki 

Kamanda wa polisi mkoani Kilimanjaro ACP Hamisi Issa amesema kwa sasa wamepata kibali cha mahakama cha kufukuwa mwili wa mwanafunzi huyo mwenye umri wa miaka 16 ambao umezikwa katika makaburi ya manispaa ya Moshi na kuhifadhiwa Mochuari kwa ajili ya uchunguzi. 

Amesema mpaka sasa uchunguzi unaendelea kubaini chanzo cha kifo cha mwanafunzi huyo pamoja na watuhumiwa wanaosadikiwa kuhusika katika kifo chake ili taratibu za kisheria ziweze kuchukuliwa dhidi yao. 

Aidha kamanda Issa ametoa onyo kali kwa wamiliki wa shule ambao wamepewa dhamana ya kulea watoto. 

Mzazi wa mtoto huyo Bw.Jackson Makundi amesema amesikitishwa na taarifa za kupotea kwa mtoto wake ambapo ameomba vyombo vya dola kufanya uchunguzi wa kina na kuwachukulia hatua za kisheria wale wote watakaobainika kuhusika na kifo hicho. 


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo