Serikali imesema
haijapuuza maagizo ya kuwapeleka watumishi katika kituo cha upasuaji cha Lupila
wilayani Makete mkoani Njombe
Akitoa majibu ya hoja
katika baraza la madiwani halmashauri ya wilaya ya Makete ya kukosekana kwa
watumishi katika kituo cha upasuaji katika kituo cha afya Lupila, Kaimu
Mkurugenzi mtendaji Bw. Gregory Emmanuel amesema tayari mtumishi mmoja
ameshapelekwa kwenye kituo hicho kwa ajili ya kazi
Amesema kutokana na
agizo la Rais John Magufuli la kutomhamisha mtumishi pasipo kumpa fedha za
uhamisho, wanalazimika kuwapeleka watumishi hao kwa awamu kulingana na
upatikanaji wa fedha ambapo pia wiki hii wanatarajia kumpeleka mtumishi
mwingine
Miezi michache
iliyopita Mkuu wa mkoa wa Njombe Christophel Olesendeka alifungua chumba cha
upasuaji katika kituo cha afya Lupila na kuagiza watumishi wapelekwe mara moja
katika kituo hicho
Sikiliza sauti hii hapa chini>>>>>
Sikiliza sauti hii hapa chini>>>>>