Manara: Hawa watanzania ni watu wa wapi? Wengi hawajui Mpira

Mkuu wa idara ya habari na mawasiliano wa Klabu ya Simba Haji Manara amesema anashangazwa na watanzania wanaoibeza Simba pale inapokuwa haijashinda mechi inazocheza

Amesema hata timu ya Simba ingewasajili Ronaldo na Mesi na Kocha akawa Sir Alex Furgerson na Kocha msaidizi akawa Jose Morinyo bado timu hiyo haitashinda kila mechi

"Mi nimekuwa nikishambuliwa sana, hasa Simba inapotoa Sare, jamani mi najiuliza hivi watanzania wanajua mpira kweli, sasa sijui ndio nawatukana lakini najiuliza hivi wanajua mpira kweli? hawa watanzania ni watu wa wapi? amesema Manara

Amesema kwa sasa wanapitiia taarifa ya Kocha wao Omog kuangalia mapendekezo yake ili waweze kufanya usajili kama itahitajika kufanya hivyo kwa mapendekezo ya kocha huyo


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo