Askari polisi watimuliwa kazi na Mkuu wa Mkoa

Askari wawili wa Jeshi la Polisi wanaofanya kazi za doria za Utalii  kisiwani Zanzibar wameondolewa  katika kitengo hicho cha doria kutokana na kujihusisha na masuala ya rushwa.
Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Kaskazini Unguja ambae pia ni Mkuu wa Mkoa Mjini Magharibi Mh. Ayoub Mahmoud amechukua hatua  baada ya uwepo wa malalamiko kwa baadhi ya wananchi  kuhusiana na tabia za rushwa.
Askari hao wamelalamikiwa kuomba na kuchukua rushwa kutoka kwa watalii katika Ukanda wa fukwe za Nungwi na kusababisha kero kwa wawekezaji wa maeneo hayo.
Wakati agizo hilo likitakiwa kuchukuliwa hatua mara moja pia Mkuu huyo ameagiza kufanyika kwa uchunguzi wa askari hao


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo