Vifaranga vya Kuku vyachomwa moto

Shehena ya maboksi ya vifaranga vya kuku iliyokamatwa ikiingizwa nchini kwa kutumia njia za panya wilayani Longido mkoani Arusha imeteketezwa chini ya uangalizi wa wataalam na watendaji wa sekta ya mifugo na kituo cha forodha cha Namanga huku wahusika wakiendelea kushikiliwa na kuhojiwa na vyombo vya dola.

Shehena hiyo ilikamatwa katika eneo la Namanga wilayani Longigo mkoani Arusha ikiingizwa nchini kwa njia za panya hatua ambayo watendaji wa kituo cha Namanga na wa idara ya mifugo mkoa wa Arusha wamesema hatua zaidi za kudhibiti vitendo hivyo zitaendelea kuchukuliwa.
Afisa Mfawidhi Mkaguzi wa mifugo Bw Medard Tarimo amesema vifaranga hivyo havikupaswa kuingizwa nchini na kwamba pamoja na kuteketezwa kwa vifaranga hivyo pia hatua zaidi zitaendelea kwa waliowezesha kufanikisha zoezi hilo na pia kwa gari lililotumika.
Kwa upande wake mtuhumiwa aliyekutwa na vifaranga hivyo vinavyokadiriwa kuwa na thamani ya zaidi ya milioni 12 amesema amevinunua nchini kenye japo hakuwa tayari kueleza alikokuwa anavipeleka.
Serikali tangu mwaka 2007 ilipiga marufuku kuingiza mayai na vifaranga kutoka nje ya nchi.



JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo