Jeshi la mwaga ajira

Jeshi la kujenga taifa (JKT) limetangaza nafasi za kazi kwa vijana ambao wanataka kujitolea katika jeshi hilo na kusema zoezi la kuchagua vijana kwa ajili ya kujiunga na jeshi hilo litaanza mwezi Novemba 2017

Mkurugenzi wa Utumishi wa (JKT) Kanali Julius Kadawi amesema kuwa nafasi za kujiunga na Jeshi hilo haziuzwi na amewataka vijana kutokubali kutoa fedha zozote ili kujiunga na jeshi hilo huku akisisitiza nafasi hizo zinaratibiwa na ofisi za Wakuu wa Wilaya na mikoa nchi nzima. 
"Zoezi la kuchagua vijana litaanza mapema mwezi Novemba mwaka huu na vijana watakaochaguliwa watatakiwa kuripoti kwenye makambi ya JKT kuanzia Disemba 4, 2017 hadi Disemba 9, 2017. Jeshi la kujenga Taifa linaendelea kusisitiza kuwa nafasi ya kujiunga na JKT haziuzwi na yoyote atakayehusika na kuuza au kununua nafasi hizo atachukuliwa hatua"alisisitiza Julius Kadawi 
Mbali na hilo Kanali Julius amesema sifa za vijana ambao wanatakiwa kujiunga na jeshi hilo na aina ya vifaa ambavyo vinatakiwa kwa wale ambao watachaguliwa zinapatikana katika tovuti ya JKT. 


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo