Spika Ndugai: Nyalandu Bado Ni Mbunge Halali

Spika wa Bunge Job Ndugai amesema hajapokea barua yoyote ya kujiuzulu ya Mbunge wa kaskazini Lazaro Nyalandu mpaka sasa

Spika Ndugai amesema anamtambua mbunge huyo kama mbunge halali kwa kuwa barua yake ya kujiuzulu bado hajaipata

Akizungumza katika mahojiano maalum na kituo cha Azam TV Spika Ndugai amesema hawezi kulizungumzia suala hilo kwa undani zaidi kwa kuwa hajapokea barua ya kujiuzulu kiongozi huyo na pia amesema ingekuwa vema angempatia barua ya kujiuzulu yeye kwanza kabla ya kutangaza kujiuzulu kwake


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo