Polisi Wanne Watiwa Mbaroni kwa Kumjrehi Mke Wa Mwenyekiti


Kamanda wa Polisi mkoa wa Mwanza, Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi, Ahmed Msangi ametoa amri kukamatwa kwa askari polisi wanne wa Kituo Kikuu cha Polisi Nyamagana kutokana na asakri hao kumjeruhi kwa risasi mke wa Mwenyekiti mtaa.

Kamanda Msangi amesema polisi hao tayari wametiwa mbaroni kwa kumjeruhi kwa risasi mguuni Bi. Editha Ntobi ambaye ni mke wa Mwenyekiti wa Serikali ya mtaa wa Majengo Mapya uliopo katika Kata ya Mabatini jijini Mwanza.

Msangi amesema polisi hao wanatuhumiwa kufyatua hovyo risasi zaidi ya 10, kuharibu mali za raia lakini pia wanadaiwa kufanya matukio hayo kutokana na kulewa wakati wakiwa kwenye doria kinyume na utaratibu wa kazi yao.

Bi Editha Ntobi ambaye ni majeruhi wa kupigwa risasi amelazwa katika hospitali ya Rufaa Bugando iliyopo jijini Mwanza kutokana na kuvuja kwa damu nyingi kufutia tukio hilo.

==>Tazama Video hapo chini( Video kwa hisani ya MillardAyo)
 


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright 2025 EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo