NAIBU WAZIRI AGAWA VITABU VYA SHULE ZA SEKONDARI JIMBONI MWAKE

 
 Makete 
                                               
Naibu waziri wa  maji ambaye pia ni  mbunge  wa Jimbo la  Makete Mh.Dr.Binilith  Mahenge, ametoa  msaada  wa vitabu zaidi ya elfu moja kwa  shule  za  sekondari zilizopo wilayani Makete.

Katika  ziara  yake  ya  siku moja wilayani hapo, Dr Mahenge ametoa vitabu 100 kwa shule ya sekondari ya Mbalatse na vingine 100 kwa  shule ya sekondari  Lupila ikiwa ni mkakati wake wa kukuza kiwango cha elimu wilayani Makete.

Dr Mahenge pia amefanya  Mikutano ya  hadhara  katika Vijiji vya Mbalatse  na Ukange huku akiwataka  wananchi Kutambua fursa  ya kutumia shule  za  sekondari za  kata na  si kutorosha  watoto kwenda  mjini kufanya  vibarua.

Hata  hivyo Naibu waziri Dr Mahenge ametembelea Hospitali ya Consolata  Ikonda ambapo alielezwa changamoto zinazoikabili  hospitali hiyo kuwa  ni pamoja  na Nishati  ya  umeme, Ambapo kwasasa wanatumia Jenereta kiasi cha kukwamisha baadhi ya  shughuli ikiwa ni pamoja na kitengo cha  mifupa.

Akijibu baadhi ya  changamoto Mh naibu waziri Dr Mahenge, amesema Baadhi ya changamoto zimeshidwa kutekelezeka  kutokana  na Ufinyu wa  bajeti ya  serikali
Na Aldo Sanga


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright 2025 EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo