Wanaume wazua Gumzo siku ya Chanjo Makete

Mgeni rasmi (kwa niaba ya Mkuu wa wilaya) Eliab Simba akimpa mtoto chanjo katika uzinduzi wa chanjo Kiwilaya(Picha/Habari na Edwin Moshi)
-----------

Imeelezwa kuwa suala la kumpeleka mtoto kliniki kupatiwa chanjo sio la Mama peke yake badala yake baba naye anawajibu wa kufanya hivyo kwa mtoto wake

Kauli hiyo imetolewa na Mkuu wa wilaya ya Makete Mh Veronica Kessy katika hotuba iliyosomwa kwa niaba yake na Afisa Mipango wilaya ya Makete Eliab Simba katika zoezi la ufunguzi wa wiki ya chanjo iliyofanyika kiwilaya Katika kijiji cha Ndulamo wilayani hapa

Amesema kumekuwa na dhana potofu iliyojengeka kwa jamii kuwamba jukumu la kuwapeleka watoto kupatiwa chanjo ya kuwakinga na magonjwa mbalimbali kuwa ni la mama peke yao jambo ambalo si la kweli na badala yake wazazi wote wawili washirikiane pamoja kuwapeleka watoto wao kupatiwa chanjo

Akitoa taarifa ya mwenendo wa chanjo Kiwilaya kwa kipindi cha januari hadi Machi mwaka huu, Kaimu Mganga mkuu wilaya ya Makete Bw. Boniphace Sanga amesema watoto waliotarajia kupata chanjo ya kifua kikuu walikuwa 1014 lakini waliochanjwa ni 881 sawa na asilimia 87

Baadhi ya wazazi waliowaleta watoto wao kupatiwa chanjo wameelezea furaha waliyonayo huku wakiwahimiza wale wenye tabia ya kutowapeleka watoto kupatiwa chanjo kuacha mara moja


Wiki ya chanjo kiwilaya imezinduliwa leo Aprili 24 na itaendelea hadi Aprili 30
 Kaimu Mganga Mkuu wilaya ya Makete Boniphace Sanga akitoa taarifa kwa Mgeni Rasmi

Mwakilishi wa Mgeni Rasmi akitoa hotuba yake

Hotuba ikiendelea
Wananchi wakisikiliza hotuba ya mgeni Rasmi




Kina mama wakifurahi baada ya watoto wao kuchanjwa na mgeni Rasmi

Ukaguzi wa kadi za watoto uiendelea kabla ya kupatiwa chanjo


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo