skip to main |
skip to sidebar
Haji Manara atoa kauli hii baada ya kipigo cha jana
Msemaji wa Simba, Haji Manara anaamini kikosi cha Simba kina nafasi ya kubeba ubingwa.
Manara anaamini Simba itabeba ubingwa kama itarekebisha makosa katika mechi tano zilizobaki.
Simba imepoteza mechi mechi yake dhidi ya Kagera Sugar kwa kuchapwa kwa mabao 2-1 wakati ilikuwa na matumaini ya kubaki kileleni hadi mwisho wa ligi.
“Ni kweli tumekosea, ni kweli tumefungwa. Hakuna haja ya kupoteza muda, tuendelee kupambana.
“Bado tuna nafasi, kikubwa tunahitaji utulivu na kurekebisha makosa,” alisema.
JIUNGE NA EDMO BLOG SASA
Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube
Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi