AUDIO+Picha: Bidhaa zilizokwisha muda wa Matumizi zakutwa zikiuzwa Madukani Makete














Idara ya afya wilayani Makete mkoani Njombe imeendesha zoezi la kushtukiza katika maduka mbalimbali katika kijiji cha Tandala na kukamata bidhaa zilizokwisha muda wa matumizi zikiendelea kuuzwa katika maduka hayo.

Akizungumza na blog hii Afisa Afya wa kata ya Tandala Bw. Huruma Mkiramweni amesema kuwa wamefanya ukaguzi huo katika kijiji cha Tandala kwa wafanya biashara na kubaini bidhaa zenye thamani ya zaidi ya shilingi laki sita zimekamatwa zikiwa zimeisha muda wake wa matumizi.

Mkiramweni anelezea sheria ambazo zitachukuliwa kwa mfanya biashara pindi anapokutwa na bidhaa zilizokwisha muda wake wa matumizi kuwa faini yake ni kuanzia shilingi laki moja hadi milioni moja

Afisa mtendaji wa kata ya Tandala Bi, Kalemela Marley amesema kuwa kutokana na ukaguzi walioufanya kwa kijiji cha Tandala wamebaini kuwa kuna baadhi   ya watu wanauza vitu vilivyokwisha muda wake wa matumizi tangu mwaka 2014 na mchakato huo utafanyika kwa kata nzima.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo