Wazawa wa Kijiji Cha Ndulamo Makete waonesha Mfano wa Kuigwa na Kila Mtu

Wazawa wapenda maendeleo kutoka nje ya kijiji cha Ndulamo Kata ya Iwawa wilayani Makete mkoani Njombe wameendelea kuunga mkono serikali na jitihada za wananchi wa kijiji hicho za ujenzi wa shule mpya ya msingi Kiduga iliyopo kijijini hapo

Kufuatia hali ya ujenzi wa vyumba vingine vitatu vya madarasa pamoja na ofisi za walimu inayoendelea shuleni hapo, wazawa hao wamechangia bati 76, misumari kilo 25, vyote vikiwa na thamani ya shilingi milioni moja laki saba na elfu themanini na moja (1,700,081)

Akitoa taarifa hiyo afisa mtendaji wa kijiji cha Ndulamo Majuto Mbwilo amesema pamoja na kuwa utawasogeza kwa kiasi kikubwa na kuwapunguzia gharama, lakini bado wanauhitaji wa michango ya wadau mbalimbali ili kazi hiyo iweze kumalizika kwa wakati

Amesema shule hiyo imeanza kutumika tayari kuanzia mwezi huu ambapo kwa kuanzia wamepewa walimu watatu, na madarasa matatu kwa maana ya darasa la awali, la kwanza na la pili ikiwa na jumla ya wanafunzi 118



Mtendaji huyo akatumia fursa hii kutoa onyo kwa wazazi au walezi ambao hawatapeleka watoto wao shule licha ya jitihada hizo zinazofanywa kuwa sheria haitawaacha

Sikiliza Sauti Hapa Chini:-


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo