Halmashauri ya Makete yahaha kuokoa Jahazi la Mawasiliano ya Barabara Ukwama Yasikatike


Halmashauri ya wilaya ya Makete mkoani Njombe hivi sasa inahaha kunusuru kukatika kwa mawasiliano ya barabara kutoka Njia Panda ya Masisiwe kuelekea Ukwama Mpaka Ihanga kutokana na uharibifu wa barabara hiyo uliosababishwa na mvua zinazoendelea kunyesha wilayani hapa

Akitoa taarifa ya hali ya barabara hiyo, Diwani wa kata ya Ukwama Mh. Agustino Tweve amesema hali ya barabara hiyo katika baadhi ya maeneo sio nzuri na endepo mvua zitaendelea kunyesha mawasiliano ya barabara hiyo yatakatika na kusababisha magari hasa basi la abiria linalokwenda Ukwama kukatisha safari zake

Amesema mpango wa kuikarabati barabara hiyo upo na tayari fedha zimeshatengwa lakini kinachokwamisha hivi sasa ni mvua zinazoendelea kunyesha, lakini pamoja na hayo wamemuomba mkandarasi atakayejenga barabara hiyo kufanya marekebisho katika maeneo korofi ili barabara hiyo iendelee kupitika

Hata hivyo diwani huyo ametaja sababu za kuharibika kwa barabara kuwa ni pamoja na kuziba mifereji ya kupitishia maji hali iliyopelekea maji kupita barabarani, pamoja na magari yenye uzito mkubwa kuliko uwezo wa barabara kupita katika barabara hiyo

Mkurugenzi wa kampuni ya Asajile Builders Limited itakayofanya matengenezo ya barabara hiyo Bw. Asajile Mbwilo amewahakikishia watumiaji wa barabara na wananchi kwa ujumla kuwa itapitika baada ya marekebisho atakayoyafanya hivi karibuni


Mkandarasi huyo ameomba ushirikiano wa kutosha kwa wananchi kwani serikali peke yake haiwezi kufanya hayo, lakini ushirikiano wa pamoja ndio utawezesha matengenezo ya barabara hiyo kukamilika huku akiwasihi wananchi kuwa mstari wa mbele kutunza miundombinu hasa barabara ili ziweze kudumu kwa muda mrefu


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo