Mwananchi wa Tandala Makete aamua Kujiua kwa Kujinyonga Usiku huu, Jionee Hapa




Makete.
Mwanaume aliyefahamika kwa jina la Bahati Marukusi Nyaluke ambaye umri wake unakadiriwa kuwa miaka zaidi ya (40 )amekutwa amejinyonga chumbani kwake jioni ya Desemba 8 mwaka huu eneo la Kilovoko kijiji cha Tandala wilayani Makete mkoani Njombe.

Taarifa kutoka eneo la Tukio zinadai kuwa mwili huo ulionwa na mwanaye ambaye ni Husseni Bahati (21) kisha kutoa taarifa kwa watu wengine.

Polisi kutoka kituo cha polisi Tandala wamefika eneo la Tukio na kufanya ukaguzi wa mwili wa marehemu kisha kutoa ruhusa ya kuushusha mwili huo kutoka kwenye kamba  ili kuendelea na taratibu zingine za jeshi hilo.

Mpaka mwandishi wa eddy blog anaondoka kwenye eneo la Tukio usiku huu Disemba 8 taarifa za kuuzika mwili wa marehemu zilikuwa hazijathibitishwa na jeshi la polisi na kwamba zitatolewa na mamalaka husika ya jeshi la polisi usiku huu ama asubuhi ya Desemba 9 kama uzikwe ama uendelee kusubiri.
Chanzo cha kifo cha marehemu bado hakijafahamika huku uchunguzi zaidi ukiendelea

Kwa taarifa za awali Marehemu inadaiwa aliingia chumba cha pili ambacho hakina Dari kisha kufunga kamba aina ya manila na akatoboa dari ya silin bodi akaitolea kamba iliyotoka kwenye kenchi na akaingia chumbani mwake na kujifungia na kufanya tukio la kutoa uhai wake.


Taarifa kamili za tuio hilo zitakujia hapa baada ya kuzipata kutoka jeshi la polisi


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo