AUDIO: Mkuu wa Mkoa wa Njombe atoa Onyo Kali kwa TANAPA, Ole wao wapige Mtu

Watumishi wanaosimamia hifadhi za taifa (TANAPA) pamoja na maeneo mengine yaliyochukuliwa na serikali kwa ajili ya hifadhi wameagizwa kuacha tabia ya kuwapa kipigo wananchi wanaozunguka maeneo yaliyohifadhiwa kwa kuwa hali hiyo inaongeza migogoro badala ya kuitatua

Kauli hiyo imetolewa leo na mkuu wa Mkoa wa Njombe Dkt Rehema Nchimbi katika kikao cha Kamati ya Ushauri ya Mkoa (RCC) kilichofanyika mkoani hapo, ambapo amesema wananchi ndio majirani wakubwa wa maeneo hayo badala ya kuwapiga wanatakiwa wawaelimishe pale wanapokosea badala ya kuwapiga kwa kuwa hali hiyo inajenga chuki na migogoro kuongezeka

Mkuu huyo ameagiza mtumishi yeyote atakayempiga mwananchi aliyekiuka sheria za hifadhi atachukuliwa hatua za kisheria hivyo kama wakiwakamata wananchi waliokosea wanatakiwa kuwapeleka kwenye vyombo vya sheria ili wachukuliwe hatua za kisheria badala ya wao kuchukua sheria mkononi kwa kuwapiga

Uamuzi huo wa mkuu wa mkoa umetolewa baada ya kupokea taarifa ya hali ya migogoro ya ardhi kwa wilaya zote za mkoa wa Njombe ambapo kwa taarifa ya mkuu wa wilaya ya Makete Mh Veronica Kessi imeeleza kuwepo kw migogoro ya ardhi katika wilaya yake ikiwemo wananchi kuwa na migogoro na hifadhi za taifa


Aidha Mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya Wanging’ombe Antony Mawata na Mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya Makete Egnatio Mtawa wamezungumzia mgogoro baina ya wilaya hizo mbili unaosababishwa na ardhi na wakaahidi kukaa pamoja kuumaliza mgogoro huo
Sikiliza sauti hapa chini:-


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright 2025 EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo