Hali mbaya kwa Scorpion, Apigiliwa msumari mwingine



Mkurugenzi wa Mashtaka(DPP) amemuongezea shtaka lingine mshtakiwa Salum Njwete maarufu kama Scorpion na sasa atakuwa na mashtaka mawili ya unyang'anyi wa kutumia silaha na shtaka la kujeruhi.

Scorpion aliongezewa shtaka hilo jana na Wakili wa Serikali Nassoro Katuga, kabla ya kumsomea Maelezo ya Awali (PH).

Baada ya kusomewa maelezo ya awali, Scorpion alikubali hoja mbili na sita kuzikana.
Kutokana na maelezo hayo, hakimu mkazi wa mahakama hiyo, Flora Haule aliahirisha kesi hiyo hadi Desemba 14, mwaka huu kesi hiyo itakapoanza kusikilizwa.

Mshtakiwa amerudishwa rumande kutokana na moja ya shtaka linalomkabili kutokuwa na dhamana.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright 2025 EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo