AUDIO: Mwanamke ageuka Tishio Ipelele Makete....Avamia Msitu wa Kijiji na Kuupasua Mbao

Mgogoro mkubwa umeibuka baina ya wananchi wa kijiji cha Missiwa kilichopo katika kata ya Ipelele tarafa ya Magoma wilayani Makete baada ya mama aliyejulikana kwa jina la Merry Mwamande kupewa idhini na mahakama ya mkoa wa Njombe kuendelea kuuvuna msitu ambao kijiji hicho kinadai kuwa kinaumiliki kihalali.

Hayo yamebainika wakati wa mkutano kati ya uongozi wa kata ya Ipelele na wananchi wa kijiji hicho uliofanyika katika ofisi ya kijiji cha Missiwa baada ya kusomwa waraka uliotoka mahakamani kuwa mama huyo aitwaye Merry Mwamande ameshinda kesi hivyo kupewa kibali cha kuendelea kuuvuna msitu huo.

Kwa mujibu wa maelezo ya baadhi ya wananchi na viongozi wa kijiji hicho wanadai kuwa mwaka 2006 waliwahi kuuza msitu huo kwa ajili ya ujenzi wa shule lakini eneo lilibaki kuwa miliki ya kijiji hicho lakini wanashangaa kuona mama huyo anaposema ni eneo lake.

Pia taarifa kutoka kwa wananchi wa kijiji hicho zinadai kuwa lilipofunguliwa jalada kuhusu kesi hiyo wananchi walikuwa wakichanga fedha na kumkabidhi mwenyekiti mstaafu anayeitwa Bw.Lingison Mbwilo ili aweze kuhudhuria kesi hiyo lakini inasemekana alikuwa haendi hivyo mahakama ikaamua kuwa eneo hilo apewe mama huyo jambo ambalo wananchi na baadhi ya viongozi wa kijiji hicho wanalilalamikia.

Kwa upande wake mwenyekiti wa mpya wa kijiji cha Missiwa aliyechaguliwa katika uchaguzi wa serikali za mitaa mwaka jana Bw.Mesaukyadi Mbola akaelezea namna alivyokabidhiwa ofisi hiyo.

Kwa upande wake Mama anayelalamikiwa aliyejitambulisha kwa jina la Merry Mwamande ambaye anaishi Ntokela wilayani Rungwe akaelezea kuhusu madai hayo.

Pia ameongeza kuwa anashangaa kuona wananchi wa kijiji hicho wanalalamikia maamuzi ya mahakama kwani walipoitwa mahakamani walikuwa hawafiki.


Diwani wa kata ya Ipelele Mh.Mwipelele Mbogela amezungumza na kituo cha redio Green fm mara baada ya mama huyo kuzungumza na mwandishi wetu na kudai kuwa msitu huo ni wa kwake na kudai kuwa haafiki anachokisema mama huyo huku akieleza hatua atakazochukua kama diwani.

Na Fadhili Lunati

Sikiliza sauti hizi hapa chini:-


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo