Kigogo wa TASAF Afutwa Cheo

Serikali imemfuta cheo mratibu wa mfuko wa maendeleo ya jamii-TASAF- wilaya ya Kinondoni Bwana Onesmo Koyamba na kulitaka jeshi la Polisi kushirikiakiana na taasisi ya kuzuia na kupambana na rushwa- TAKUKURU kuchunguza tuhuma zinazomkabili ikiwemo upotevu wa zaidi ya shilingi milioni 266 zinazodaiwa kupewa wananchi masikini hewa.

Agizo hilo limetolewa na mkuu wa wilaya ya Kinondoni Bwana Ali Hapi wakati akizungumza na waandishi wa habari, ambapo amesema mbali na tafiti kuonyesha  kaya masikini hewa 537 kulipwa kiasi hicho cha fedha, uchunguzi umebaini majina ya watumishi wa serikali na wafanyabiashara  zaidi ya 517 wameshalipwa zaidi ya shilingi milioni 180.3 na kusisitiza tayari uamuzi umeshafanyika wa kuondoa orodha ya majina hao katika kunufaika na fedha hizo na kuwafikisha katika mikono ya sheria.

Aidha Bwana Hapi ameshauri mamlaka  husika kuangaliwa  upya mfumo na upatikanaji wa wananchi walengwa wanaotakiwa kunufaika na fedha hizo, taratibu za ulipaji wa fedha na mfumo wa usimamizi ili kudhibiti upotevu wa fedha,huku mtendaji  kata ya Kinondoni Bwana  Amiri Bakari ametaka kuwepo kwa utaratibu rasmi wa wazi utakaoanzia katika ngazi ya chini ya serikali ya mtaa ili kuhakiki hali ya umasikini kwa walengwa pamoja na idadi.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo