Wanaume Njombe wataja sababu za Kuogopa Kutahiriwa

NJOMBE.
Wakazi  Wa wilaya ya Wanging'ombe mkoani Njombe wameiomba serikali kuwasogezea karibu huduma ya kituo cha afya ili baadhi ya wanaume ambao hawajafanyiwa  tohara waweze kupatiwa huduma hiyo kwani baadhi yao wamekuwa wakidai huduma zipo mbali hivyo wanashindwa kufika huko.

Ombi hilo limeombwa na baadhi ya wanaume ambao hawajafanyiwa tohara katika kijiji cha Itowo kata ya Mdandu wilayani Wanging'ombe ambao wamemweleza  mhamasishaji wa eneo hilo kuwa wanashindwa kwenda kufanyiwa tohara kutokana na umbali uliopo hadi kufika katika hospitali ya Kibena Njombe ambako huduma hiyo pia inapatikana.

Akizungumza na mwandishi wa Green Fm Grace Sanga, mmoja wa waelimishaji hao amesema kuwa hivi sasa muamko wa wanaume kwenda kufanyiwa tohara umekuwa mkubwa kutoka na elimu inayoendelea kutolewa kwa wanaume kuhusu faida na hasara za kutofanya  tohara.

Pia imeelezwa kuwa kumekuwa na baadhi ya  changamoto mbalimbali kwa baadhi ya wanaume  kama vile kuogopa kufanyiwa tohara kipindi cha msimu wa joto kwa Imani kuwa vidonda vitachelewa kupona, na wengine wakiamini kuwa baada ya kufanyiwa tohara nguvu za kiume zitapungua  hivyo kuwafanya washindwe

Hivyo  wanaume ambao bado hawajafanyiwa tohara wametakiwa kuachana  na Imani potofu na kushauriwa kuchukua hatua ili kujikinga wao pamoja na wenza wao na maradhi yanayosababishwa na kutofanyiwa tohara.


Na Grace Sanga


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo