Changamoto za Kijiji Cha Usililo Makete zamuibua Mtendaji

Wananchi wa kijiji cha Usililo kilichopo kata ya Luwumbu wilayani Makete mkoani Njombe wameaswa kuwa mstari wa mbele katika kufanya shughuli za kimaendeleo ili kukiinua kijiji hicho ikizingatiwa bado kiko nyuma kimaendeleo.

Akizungumza na mwandishi wa habari hii Asukile Mwalwembe, Afisa Mtendaji wa kijiji hicho Bi Victoria Sangu amesema wanamikakati mingi katika kuhakikisha wanapiga hatua kimaendeleo na kuomba wananchi wampe ushirikiano.

Pia Afisa mtendaji huyo amesema kuwa kama wananchi wa kijiji hicho wataendelea kutoa ushirikiano watakisogeza mbele kijiji chao na kuomba waandishi wa habari kuendelea kutoa ushirikiano katika kutoa hamasa kwa wananchi hao kujitokeza katika shughuli za maendeleo.


Bi Sangu amesema kuwa wananchi wengi wa kijiji hicho cha Usililo wanajitokeza kwa wingi Kushiriki shughuli za maendeleo licha ya baadhi ya watu kutojitokeza ingawa wanawachukulia hatua na kuongeza pia hawaingizi itikadi za kisiasa katika kufanikisha suala la maendeleo.

na Asukile Mwalwembe


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo