Hatua za ujenzi wa barabara ya Makete Njombe kwa kiwango
cha lami zimeendelea kutekelezwa, baada ya uongozi wa kijiji cha Tandala
Wilayani Makete kuutangazia umma hatua wanazotakiwa kuzifanya kuanzia Jumatatu
Ijayo ili kupisha ujenzi wa barabara hiyo
Taarifa iliyotolewa na Kaimu Afisa Mtendaji wa kijiji Cha
Tandala Bw. Bruno Mhiche imewataka wananchi wote waliojenga ndani ya mita 22.5
toka katikati ya barabara ya Makete Njombe kufika katika ofisi za Kijiji hicho
kwa lengo la kupokea taarifa rasmi kutoka TANROADS za kupisha ujenzi huo
Mwenyekiti wa kijiji cha Tandala Andowise Memba
akizungumzia hatua hiyo, amewataka wananchi hasa wahusika kutoa ushirikiano kwa
serikali kwa lengo la kupewa utaratibu wa kupisha ujenzi huo kama ambavyo serikali
imetangaza
Katika kipindi cha mwaka huu wa fedha 2016/2017 serikali
kupitia wizara ya ujenzi uchukuzi na mawasiliano tayari imetangaza Ujenzi wa
barabara ya Makete Njombe kwa kiwango cha lami