Katika kuendeleza juhudi za kutatua tatizo la maji katika
Kijiji cha Tandala wilayani Makete Mkoani Njombe, Mkutano wa dharura wa kijiji
hicho umeunda timu maalum kwa ajili ya kufanikisha kuondokana na tatizo la maji
kijijini hapo
Timu hiyo iliyoundwa imehusisha wajumbe wawili kutoka
Kila kitongoji cha Kijiji hicho, na hali hiyo inafuatia majadiliano ya pamoja
na wananchi hao katika mkutano wa hadhara uliofanyika leo ukiwa na ajenda moja
ya kujadili kero ya maji
Mwenyekiti wa kijiji hicho Andowise Memba akaanza kwa
kuufungua mkutano huo na kueleza lengo lake
Diwani wa kata hiyo Mh Egnatio Mtawa amewataka wananchi
hao kutambua kuwa suala la ukosefu wa maji linamhusu kila mtu, na sehemu nzuri
ya kusemea ni katika mikutano ya hadhara
Baadhi ya wananchi waliohudhuria mkutano huo wakatoa
mapendekezo yao namna ya kuondokana na kero hiyo ya maji kabla ya kupatiwa
elimu ya kuupata uongozi wa kushughulikia maji kutoka kwa mtaalamu wa Idara ya
Maji kutoka halmashauri ya wilaya ya Makete
Katika hatua nyingine akizungumza katika Mkutano huo
Diwani wa kata hiyo Mh Mtawa amewaambia wananchi kuhusu umuhimu wa kutunza
vyanzo vya maji na kusema hatakuwa na huruma na wale wanaochezea vyanzo vya
maji vilivyopo katika kata yake