Mbunge Norman Sigalla Akanusha Kupokea Mishahara hewa....Ataja Hela aliyoingiziwa kwenye akaunti

Baada ya kuenea kwa taarifa za Mbunge wa Makete (CCM), Profesa Norman Sigalla ambaye alikuwa Mkuu wa Wilaya ya Songea kupokea mshahara wa ukuu wa wilaya kwa miezi mitano huku akiwa tayari ameshaachana na kazi hiyo – mwenyewe amefafanua juu ya taarifa hizo.
Profesa Sigalla alitoa maelezo hayo jana alipofika ofisi za gazeti la Mwananchi ambao ndiyo walitoa taarifa hizo hapo awali za Mbunge huyo kupokea mishahara hewa.
Mbunge huyo amekanusha kiasi cha fedha kilichoingia kwenye akaunti yake kwamba si shilingi milioni 23 kama baadhi ya taarifa zinavyodai bali ni shilingi milioni 5,091,734.96 ndizo zilizoingizwa kwenye akaunti yake ya benki.
Profesa Sigalla amedai kuwa hali hiyo ilitokana na makosa ya ofisa utumishi wa ofisi ya katibu tawala wa Mkoa wa Ruvuma kumrudisha kwenye orodha ya malipo ya mshahara kimakosa jambo ambalo alilitolea taarifa mapema kabla hata vyombo vya habari havijaipata taarifa hiyo.
Hata hivyo Mbunge huyo amekiambia kipindi cha Clouds 360 cha Clouds TV kuwa kwa sasa hali ni shwari.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo