Audio:Halmashauri ya Makete Hatarini Kukumbwa na Uhaba mkubwa wa Watumishi

Imeelezwa kuwa baada ya muda si mrefu huwenda halmashauri ya wilaya ya Makete mkoani Njombe ikakumbwa na uhaba wa watumishi kutokana na zoezi la uhakiki wa watumishi linaloendelea kufanywa na serikali

Akijibu hoja ya Mh Ilomo iliyoibuliwa katika baraza la madiwani wa halmashauri hiyo kuhusu upotevu wa mapato ya kata ya Kigala kutokana na kukosekana watendaji Afisa utumishi na Utawala wilaya ya Makete Bw. Nicodemus Tindwa amesema kutokana na zoezi la uhakiki wa vyeti linaloendelea sasa, lemepelekea serikali kusimamisha ajira zote hivyo wapo pia watumishi watakaokosa sifa kutokana na zoezi hilo ambalo bado linaendelea

Amesema anatambua ukosefu wa watendeji wa vijiji vya Kinyika na Ndapo lakini hana uwezo wa kuwapeleka watumishi wapya kwa sasa mpaka hapo serikali itakapotoa kibali cha ajira za watumishi

Wakati huo huo halmashauri kupitia baraza hilo la madiwani imetolea ufafanuzi wa matumizi ya sheria ya mazingira inayokataza kufanyika shughuli za kibinadamu katika vyanzo vya maji, kingo za mito, mabwawa, maziwa na bahari ndani ya mita 60, ambapo afisa mazingira Raphael Kalongola amesema mpaka sasa mita 60 zipo palepale ingawa wapo kwenye hatua za kumuandikia barua waziri wa mazingira kuomba utekelezaji wa sheria hiyo kwa Makete ubadilishwe


Wakati huu ambapo yanasubiriwa majibu ya waziri Kuhusu ombi hilo sheria ya sasa ya mazingira bado ipo palepale na inaendelea kutukima na kutekelezwa kama ilivyo. sikiliza sauti hapo chini


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright 2025 EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo