Salamu za Rambirambi kutoka CHADEMA kuhusu tetemeko la Ardhi Kagera

CHADEMA kinatoa salaam za pole kwa wananchi wote walioathirika na tetemeko la ardhi katika maeneo ya mikoa ya Kagera, Mwanza, Tabora na kwingine, tukio ambalo limesababisha vifo vya watu, majeruhi na uharibifu mkubwa wa mali.

Kupitia taarifa hii, chama kinatoa wito kwa Watanzania wote katika maeneo yaliyopatwa na tetemeko hilo na wengine kutoka nje ya sehemu hizo, kuguswa na tukio hilo na kuwiwa kuwasaidia waathirika wa tukio hilo katika wakati huu mgumu wa kukabiliana na athari zilizotokana na janga hilo.

Viongozi wa chama katika ngazi mbalimbali, wabunge, madiwani na wanachama wote wa CHADEMA wataungana na kusaidiana kwa kila hali na wote walioguswa na tukio hilo katika wakati huu mgumu wa kupoteza ndugu, jamaa, marafiki, kusitiri miili ya marehemu, kuuguza majeruhi na kupata hifadhi mbalimbali kwa waliopoteza mali na makazi.

Tunamwomba Mwenyezi Mungu azilaze roho za marehemu mahali pema na tunawatakia uponaji wa pole na haraka majeruhi wote wa tukio hilo.

Imetolewa Jumamosi, Septemba 11 na;
Tumaini Makene
Mkuu wa Idara ya Habari na Mawasiliano
CHADEMA


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo