Aliyekuwa Mkurugenzi wa NIDA kuendelea kusota Rumande, Mahakama yatupilia mbali dhamana


Mahakama Kuu kanda ya Dar es Salaam imetupilia mbali ombi la dhamana kwa washitakiwa sita akiwemo aliyekuwa mkurugenzi wa mamlaka ya vitambulisho vya Taifa NIDA Bwana Dickson Maimu wanaotuhumiwa kwa makosa ya kuisababishia hasara serikali ya zaidi ya shilingi bilioni 1.2.

Maamuzi hayo ya mahakama kuu yamesomwa na msajili wa mahakama kuu Projestus Kayoza ambaye amesema mahakama imefikia maamuzi hayo baada  kubaini mapungufu katika hati ya kiapo, iliyowasilishwa mahakamani hapo kwa ajili ya maombi ya dhamana,

Ameiambia mahakama kuwa maombi ya sasa ya dhamana kwa watuhumiwa hao sita yamebainika kuwa  na mapungufu kadhaa  ya  kisheria  ambapo  pia yaliombwa katika kiapo ambacho  kimebainika kuwa na mapungufu, na hivyo kuamua kutupilia  mbali  ombi  la  dhamana  kwa vigogo hao waliokuwa wakishikilia  nafasi za  juu za uongozi katika mamlaka ya vitambulisho vya Taifa.

Awali  akisoma  maamuzi kuhusu mabishano ya kisheria kuhusu kasoro zilizopo kwenye kiapo cha maombi ya dhamana kilichowasilishwa na upande wa utetezi wa watuhumiwa na kupigwa vikali na mawakili wasomi wa serikali wakiongozwa na Fredrick Mayanda, msajili huyo  wa  mahakama amesema  miongoni mwa  mapungu yaliyobainika  katika  kiapo hicho ni ukosefu wa chanzo  cha taarifa  ambazo  ziliwasilishwa na  wakili wa watuhumiwa hao Michael Ngaro.

Washitakiwa hao wanaoshitakiwa chini ya sheria ya uhujumu uchumi kwa kuisababishia serikali hasara  ya zaidi ya shilingi bilioni 1.Ambao  bado wanaendelea kusota mahabusu  kwa kukosa  dhamana  ni  pamoja na  aliyekuwa mkurugenzi mtendaji wa mamlaka hiyo, Bw  Dickson Maimu.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo